Msanii wa Hip Hop Bongo, Bill Nas amekuwa akihusishwa na biashara haramu kutokana na kushoot video kali na za gharama tofauti na hela aliyoipata mpaka sasa kwenye muziki wake.

Rapper huyo amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio, “Wasanii wengi hatupendi kuwekeza kwenye vitu vyetu.”
“Mimi nasoma biashara na elimu ya kwanza unapopata hela kwanza wekeza, unasave halafu kile kinachobakia unaweza uka-spend. Kwahiyo mimi bado nawekeza kwenye muziki wangu bado sijaanza kuspend kwa sababu naipenda kazi yangu,” ameongeza.
“Hata kwenda kushoot video Afrika Kusini nina risk sana kwa sababu siyo kama hela hizo zinarudi.”
Mpaka sasa Bill Nas ameshaachia nyimbo tatu huku wimbo wake wa ‘Chafu Pozi’ ukizidi kufanya vizuri kwenye radio na TV.
No comments:
Post a Comment