Friday, July 22, 2016

MICHEZO Dalili nyingine ya kuwa Paul Pogba atatua Man United msimu huu



Klabu ya Manchester United inayofundishwa na kocha mreno kwa sasa Jose Mourinhoimerudi kwenye headlines baada ya July 21 kutoa namba za jezi watakazovaa wachezaji wake kwa msimu wa 2016/2017, Man United wametangaza namba hizo za jezi na kuiacha namba ambayo inaaminika kuwa katengewa Paul Pogba.
Man United ambayo usiku wa July 20 iliripotiwa na na The Sun kuwa imekubaliana naJuventus ya Italia kumsajili kiungo wa kimataifa wa Ufaransa Paul Pogba kwa dau la pound milioni 105, inatajwa kuacha jezi namba 6 wazi, kitu ambacho kinatsirika kuwa ni namba ya jezi ambayo kawekewa Paul Pogba.
Manchester-United-Squad-Numbers-1024x1024
Wachezaji wapya wa Man United wote washapewa namba za jezi kama Zlatan Ibrahimovic atavaa jezi namba 9 iliyokuwa inavaliwa na Anthony MartialEric Baillyatavaa jezi namba 3 na Henrikh Mkhitaryan atavaa jezi namba 22. Pogba wakati anaondoka Man United 2012 alikuwa akivaa jezi namba 42.





No comments:

Post a Comment

Powered By Blogger